Friday, September 3, 2010

VAZI LIPI LAFAA HASA KWENDEA KANISANI? TUELIMISHANE

Wapendwa jamani hili ni jambo ambalo linawasumbua sana watu wengi na wengine hata wanadiriki kutokwenda kanisani siku nyingine sababu kubwa sina nguo ya kuvaa. Naomba tusaidiane tuelimishana kuhusu hili kwa sababu mimi ninaamini kuwa Mungu wetu haangalii mavazi  umbo, utajiri wala chohote kiwayo chote ila yeye anaangalia MOYO wako. 1Samweli 16:7

Sasa je ni vyema kwa waumini kumnyooshea kidole mtu aliyevaa nguo fupi au suruali au jeans akaenda nayo kanisani? (naongelea kwa mwanamke) Mfano kama nimeokoka nikivaa jeans kanisani au nguo fupi na (kijana wa kiume) akavaa suruali chini ya makalio inamaanisha kuwa mimi sijaokoka? Unawezaje basi kutambua kuwa mimi nimeokoka au la kwa kuangalia mavazi yangu? Au kama hata sijaokoka mimi ni muumini wa kawaida napenda kwenda kanisani napenda kujifunza kuhusu neno la Mungu je utanitenga na kuanza kunisengenya kuniangalia jicho pembe kuwa mimi sifai kuingia kanisani kwa kungalia uvaaji wangu? Je Yesu alikuja kutafuta walio watakatifu tu au wenye dhambi? Si vyema mimi nije kama nilivyo ili niweze kupata badiliko la kweli? Je si Roho Mtakatifu pia aamuaye ndani ya mioyo yetu namna ya kuwa Mtakatifu nadhani akiwa ndani yako atakuonyesha jinsi ya kuvaa au mwasemaje wapendwa?
Naomba tusaidiane kuchangia hii mada ili tujifunze na tuelimishane kusudi tupate kupona. Pia kama unazo picha za kuonyesha vazi la kwendea kanisani tafadhali naomba unipostie ili tubadilike. Barikiwa na Bwana

MAOMBI YANGU KWAKO SIKU HII YA LEO

Bwana Mungu wetu Mfalme wa Amani, ninakutukuza ninakupa heshima na utukufu. Asante kwa kuwa mwema kwetu na uaminifu wako ndani ya maisha yetu.Asante kwa kutupa kibali katika siku hii nzuri na njema ya leo. Wabariki wana wako baba panda kitu kipya ndani ya maisha yao siku hii ya leo. Bariki kazi za mikono yao, wabariki kila waingiapo na watokapo, chochote watakachofanya au kugusa kwa siku hii ya leo kiwe kimebarikiwa. Waepushe na kila hila za yule mwovu na kazi zake, waondolee magonjwa, hofu, huzuni, kukosa amani, uchungu. Wape furaha ya kweli, amani itokayo kwako, tabasamu la kweli kutoka ndani ya mioyo yao, panda ujasiri wako ndani yao. Roho Mtakatifu wape hekima itokayo kwako, maarifa  na ufahamu wako. Linda familia, watoto na ndoa zao. Nashukuru baba kwa maana maombi haya yamepata kibali machoni pako katika jina la mwanao mpendwa Yesu Kristo. Amen, Amen, Amen.

I SAID MY PRAYER FOR YOU TODAY

I said my prayer for you today and i know God must have heard; I felt the answer in my heart although he spoke not a word. I didn't ask for wealth or fame ( i knew you wouldn't mind) I asked for priceless treasures rare of a more lasting kind. I prayed that he'd be near to you and protects you at the start of each new day.
To grant you health and blessings fair and friends to share your way. I asked for happiness for you in all things great and small, but that you'd know his LOVING, CARE.
I PRAYED THE MOST OF ALL. HAVE A BLESSED DAY.