Thursday, September 23, 2010

Huduma ya Living Water Centre Ministry

Je waifahamu Living Water Centre Ministry iliyopo Kawe Dar Es Salaam.
Kutana na watumishi wa Mungu wapakwa mafuta wa Bwana ambao Roho Mtakatifu anawatumia kweli kweli. Kwa habari zaidi mafundisho sahihi ya neno la Mungu maombi na maombezi basi fika kanisani LWC upate kubarikiwa, kufunguliwa na upate kuijua kweli na hiyo kweli ikuweke huru.

Mtumishi wa Mungu Aunty Peace akiombea
















Maombezi yakifanyika kanisani LWC


Maombezi yakiendelea kanisani LWC - Makuti Kawe

Karibu katika huduma ya Living Water Centre:

RATIBA NA MATUKIO MUHIMU YA LIVING WATER CENTRE MINISTRY
Tarehe: 26/09/2010
Muda kuanzia: Saa Tatu na Nusu Asubuhi
Tukio : Ibada ya Neno na Kusifu
Mahali : Kanisani, Living Water Centre - Kawe

Tarehe: Kila siku za Alhamisi
Muda kuanzia: Saa Nne Usiku
Tukio : Mkesha Maalum kwa Mabinti - Na. Mchungaji Paschal.
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe


Tarehe: Kila siku za Ijumaa
Muda kuanzia: Saa Nne Usiku
Tukio : Mkesha Maalum kwa Vijana wa Kiume- Na. Mchungaji Paschal.
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe


Tarehe: Kila siku za Ijumaa
Muda kuanzia: Saa Saba Mchana (1:00pm)
Tukio : Ibada ya Mjini Dar Es Salaam, kwa Wafanyakazi na Wenyeji wote.
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe


Tarehe: Kila siku za Jumanne
Muda kuanzia: Saa Nne Asubuhi hadi Saa Sita na Nusu (10:00am - 12:30pm)
Tukio : Darasa la kuukulia wokovu, Maombezi na ushauri wa Mtu mmoja mmoja hadi saa 11.Jioni.
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe


Tarehe: Kila siku za Jumatano hadi Ijumaa
Muda kuanzia: Saa Tisa Alasiri hadi Kumi na Mbili jioni (3:00pm - 6pm)
Tukio : Mazoezi ya Timu ya Kusifu na Kuabudu
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe


Tarehe: Kila siku ya Ijumaa ya Mwisho wa Mwezi
Muda kuanzia: Saa Nne Usiku (10:00pm - asubuhi)
Tukio : Mkesha wa Vijana Wote
Mahali : Kanisani, LWC-Makuti, Kawe



WOTE MNAKARIBISHWA USIKOSE!!!

NENO KUTOKA KWA MAMA LILIAN NDEGI

LIVING WATER CENTRE - MAKUTI KAWE


Ibada ya Jumapili: 12/09/2010 -: Maisha ya Kuongozwa na Roho Mtakatifu
Fuatilia Mfululizo wa somo hili kwenye Website ya Kanisa.

...Ashukuriwe Mwenyezi Mungu kwa kutupa Waamini sisi tulio mwamini, Kiongozi ambaye wakati wote nia yake ni kutufikisha katika burudiko la kweli. Sisi tukiwa kama binadamu, tumeumbiwa kuongozwa na utawala fulani katika maisha yetu. Katika hali yoyote, binadamu lazima aongozwe na utawala mmoja kati ya Utawala wa Giza uliotawaliwa na Dhambi na Mauti, au Utawala wa Nuru, uliotawaliwa na Uzima wa Milele na Bududiko la kweli katika Kristo Yesu. Utawala wa Nuru, ni utawala wa Roho Mtakatifu ndani ya Maisha ya Mwamini. Utawala wa Roho Mtakatifu, wakati wote ni utawala wa faida, ni utawala uliojaa Upendo usio kifani, na gharama yake hailinganishwi na kitu chochote, kiwe Fedha, Dhahabu n.k. Ni utawala wenye ukamilifu katika kila idara ..
Fuatilia Somo letu la jumapili iliopita, lenye kichwa cha Somo "Maisha ya kuongozwa na Roho Mtakatifu" kama lilivyoletwa kwetu na Mtumishi wa Mungu Mama Lilian Ndegi.

RATIBA NA MATUKIO MUHIMU YA LIVING WATER CENTRE MINISTRY
Tarehe: 26/09/2010
Muda kuanzia: Saa Tatu na Nusu Asubuhi
Tukio : Ibada ya Neno na Kusifu
Mahali : Kanisani, Living Water Centre - Kawe >>ratiba zaidi >>
Pia, muda si mrefu tutapatikana katika Facebook na Twitter