Tuesday, November 9, 2010

MANENO YA KINYWA CHA NABII ZEKARIA YATIMIA

BWANA WA MAJESHI ASEMA HIVII,

Itatokea halafu ya kwamba watakuja mataifa na wenyeji wa miji mingi, wenyeji wa mji huu watauendea mji huu, wakisema, Haya! twendeni zetu kwa haraka tuombe fadhili za Bwana, na kumtafuta Bwana wa Majeshi, Mimi nami nitakwenda. Naam, watu wa kabila nyingi na mtaifa hodari yatakuja Yerusalem, kumtafuta Bwana wa Majeshi, na kuomba fadhili za Bwana. Bwana wa Majeshi asema hivii, Siku hizo watu kumi, wa lugha zote za mataifa, wataushika upindo wa nguo yake yeye aliye Myahudi, naam wataushika wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi kwa maana tumesikia ya kwamba Mungu yu pamoja nanyi.

Je haya maono ya Nabii Zekaria yametimia? Kwani ukiangalia kwa sasa watu wengi wanakimbilia Israel. Watumishi wa Mungu mbalimbali wanaandaa safari za watu kwenda kuona na kuomba fadhili Israel. Mataifa hodari nayo yanaitetea Israel kwa maana wamejua kuwa Mungu yupo pamoja na wana wa Israel, je ni kwamba unabii alioutoa mtumishi wa Mungu Nabii Zekaria unatimia? Tutafakari njia zetu tugeuke tutafute uso wa Bwana kwani nyakati za mwisho zimekaribia. Mpendwa fanya hima usibaki nyuma tafuta sana kuuona mkono wa Mungu ndani ya maisha yako. Mimi na nyumba yangu hatukubali kubaki nyuma wewe jeee?

MAJINA YA MUNGU

  1. ELOHIM : The Creator

  2. EL ELYON : The God Most High

  3. EL ROI : The God Who Sees

  4. EL SHADDAI : The All Sufficient One

  5. ADONAI  : The Lord

  6. JEHOVAH : The Self-Existent One

  7. JEHOVAH JIREH  :  The Lord Will Provide

  8. JEHOVAH RAPHA  :  The Lord Who Heals

  9. JEHOVAH NISSI  :  The Lord My Banner

10. JEHOVAH MEKODDISHKEM : The Lord who Santifies You

11. JEHOVAH SHALOM  :  The Lord is Peace

12. JEHOVAH SABAOTH  : The Lord of Hosts

13. JEHOVAH RAAH  :  The Lord My Shepherd

14. JEHOVAH TSIDKENU  :  The Lord Our Righteousness.

15. JEHOVA SHAMMAH  :  The Lord is There.

MAVAZI YA VIJANA WA LEO




Sijui ni kwanini vijana wetu wanapenda kuvaa style hii na sijui ni nani aliyeanzisha na kwa sababu gani kwani inamfanya kijana aonekana kuwa ni kijana mhuni hata kama hana tabia za kihuni. Juzi nilikutana na kijana mdogo kweli kweli wa miaka kama tisa kumi, alikuwa amesuka nywele zake mwenyewe na yeye kavaa style hii sema ya kwake ilikuwa imeshuka zaidi yuko na mama yake. Nikamwangalia nikajaribu kuchunguza nijue ameishikilia na nini hiyo suruali kwani ilikuwa inaonekana kama inadondoka vile lakini wapi alikuwa kama anapata shida kutembea maana anajaribu kuibalance nadhani isidondoke au ndio miondoko yenyewe kwa kweli sikupata jibu, lakini mwenyewe alikuwa anajiona yuko sawa na mama naye alikuwa anaona ni jambo jema tu. Nikatamani ni mwambie ndugu mwambie mtoto avae vizuri sema nikaona hayo maneno ningepewa hapo ningelazwa hospitali kwani wa dada black american kwa kuongea mhuu mzaramo haoni ndani. Nilichofanya ni maombi tu ya kimya kimya sina zaidi. Tuzidi kuwaombea watoto wetu wote awe msichana awe mvulana wote wanahitaji maombi ya haswa bila kuzembea.

picha kwa hisani ya issa michuzi