Wednesday, November 10, 2010

MAJINA YA MUNGU YANAVYOWEZA KUTENDA NDANI YA MAISHA YETU

Mungu anayo majina mengi tofauti tofauti ambayo ukiyatumia yanakuwa ni msaada katika maisha yako. Katika Post yangu ya nyuma nilitoa majina 15 tu ya Mungu lakini yapo majina mengine mengi ambayo ni 365 kwa maana kuwa majina ya Mungu yako sawa sawa na siku 365 yaani mwaka mzima ni sisi tu tujue ni wakati gani tunatakiwa kuyaita na kuyatumia .

Kwani wakati nikiwa na uhitaji / shida na kimbilia kuita Jehovah-Jireh yaani Mungu anayetoa kadri ya uhitaji wangu. Ukisoma Wafilipi 4:19 Paulo anawaandikia watakatifu wa Kristo Yesu walioko Filipi akiwashukuru kwa wao kumpelea msaada wa vitu mbalimbali na kuwaambia kuwa Mungu ambaye yeye ni mtoaji / mgawaji wa vitu atawapatia yale yaliyo hitaji la mioyo yao.
Hivyo basi ukiwa na shida ukiwa na uhitaji ndani ya maisha yako basi ujue kuwa yuko Mungu ambaye yeye anaoutoshelevu wote ambaye amekamilika katika kila nyanja ni mimi na wewe kujitoa kwa kuliita tu hili jina lake katika maombi yetu nae anafanya /anatugawia.
Nikipatwa na mashambulizi ya magonjwa yaletwao na yule mwovu naiita jina la Jehova Rafa yaani Mungu mponyaji. Soma 2korintho 4:7-17 magonjwa yanaletwa na hofu, uchungu kutokusamehe haya yote kwa pamoja ndio yanayofanya miili yetu kuwa dhoofu Mtume Paulo anasema hivi ktk mstari 8-10 kuwa hata tukipwata na jambo gani miili yetu inatiwa nguvu kwani kwa kufa kwake Yesu Kristo pale msalabani ni ili miili yetu itiwe uzima, kwani aliyabeba madhaifu yetu yote na kwa kupigwa kwake sisi tumepona pia ukisoma kwenye mstari wa 16 tunaambiwa kuwa hatulegei kwa kuwa utu wetu wa nje unapochakaa utu wetu wa ndani unafanywa upya kwa hiyo tusichoke kumwiita Jehova Rafa maana yeye anaanza uponyaji wa ndani halafu anakuja nje na hii itakufanya kuwa kiumbe kipya kabisa.
Pale ninapokwa na mashaka / hofu kuu imenitawala ndani ya maisha yangu basi liko jina kuu niitalo Jehova Shalom yaani Mungu wa Amani. Soma Yohana 16:33 Bwana Yesu alikuja kuleta upatanisho kati yetu sisi na Mungu na pia kuleta amani kwani yeye ni mfalme wa amani ukiwa naye hakuna shaka ndani ya maisha yako japo Yesu anatumbia ktk mstari wa 33b kuwa hapa ulimwenguni dhiki zimo na zitatupata lakini tuwe imara tusikate tamaa kwani kama yeye ameushinda ulimwengu na sisi tutashinda vita. Alikuja ulimwenguni kuleta Amani.
Ninapokuwa mpweke sina mahali pa kukimbilia ninalo jina ninalokimbilia kuliita nalo ni Jehova Shama yaani Mungu ambaye yupo. Mungu yupo kila mahali, kila wakati, kila siku milele na milele hivyo hakuna haja ya kuwa mnyonge, mkiwa kwani yeye yupo na anasikia ukisema naye anakujibu, ukimtafuta unampata. Anakusubiri tu uliite jina lake naye anasema niko hapa anakupa pumziko la moyo la kweli upweke hautakuwepo tena. Mungu wetu yupo jana, leo, kesho hata milele.
Mungu wetu ni Mungu mkuu mwenye uweza wote mwenye upendo usiopimika anatujua sisi kabla hata ya misingi ya ulimwengu kuwepo alitujua hata kabla hatujazaliwa anajua kila jambo katika maisha yetu yeye anaona mwisho tangu mwanzo hivyo ni sisi kujifunza kuliita jina lake kila wakati kutokana na uhitaji wetu .
Ukisoma Ufunuo Wa Yohana 1:8 unasema hivii MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, ASEMA BWANA MUNGU, ALIYEKO NA ALIYEKUWAKO NA ATAKAYEKUJA , MWENYEZI.
Tujifunze kumtegemea Mungu katika mambo yetu yote, si wakati wa dhiki tu hata kwenye furaha.

JE WAJUA KUWA UNAMWIBIA MUNGU?

BWANA MUNGU ANASEMA HIVII,

Tokea siku za Baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa Majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi kwa namna gani?
JE MWANADAMU ATAMWIBIA MUNGU? LAKINI NINYI MNANIIBIA MIMI, MWASEMA TUMEIBA KWA NAMNA GANI? MMENIIBIA DHAKA NA DHABIHU. NINYI MMELAANIWA KWA LAANA, MAANA MNANIIBIA MIMI, NAAM TAIFA HILI LOTE.
LETENI ZAKA KAMILI GHALANI, ILI KIWEMO CHAKULA KATIKA NYUMBA YANGU, MKANIJARIBU KWA NJIA HIYO, ASEMA BWANA WA MAJESHI MJUE KAMA SITAWAFUNGULIA MADIRISHA YA MBINGUNI NA KUWAMWAGIENI BARAKA, HATA ISIWEPO NAFASI YA KUTOSHA AU LA. NAMI KWA AJILI YENU NITAMKEMEA YEYE ALAYE, WALA HATAHARIBU MAZAO YA ARDHI YENU, WALA MZABIBU WENU HAUTAPUKUTISHA MATUNDA YAKE KABLA YA WAKATI WAKE KATIKA MASHAMBA ASEMA BWANA WA MAJESHI. NA MATAIFA YOTE YATAWAITENI HERI, MAANA MTAKUWA NCHI YA KUPENDEZA SANA, ASEMA BWANA WA MAJESHI. Soma Malaki 3:7-12

Mpendwa katika Bwana Je wewe umeshaona jinsi gani ambavyo unamwibia Mungu? Umeshaona ni kwa jinsi gani basi neno la Nabii Hagai 1:5:7 linavyotenda kazi ndani ya maisha yako? Kwani Nabii Hagai anakwambia hivii zitafakarini njia zenu, Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo, mnakula lakini hamshibi............ na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka toboka.
Unaona sasa ni kwa jinsi gani unavyokuwa haufanikiwi? Jibu ni kwamba umemwibia Mungu hivyo na yeye hakuweza kumkemea yule adui alae mshahara wako, mazao yako, kazi yako ya mikono inakuwa haisongi mbele kwa sababu umemwibia Mungu. Tubadilike wapendwa tuanza kutoa zaka zilizo kamili ili Bwana Mungu wetu atufungulie madirisha ya mbinguni tupate baraka na pia amkemee yule adui alae asiguse kazi zetu za mikono.
Naamini kwa somo hili japo nimefafanua kidogo litakujenga na kukufanya ubadilike na kuanza kutoa zaka na dhabihu kwa Mungu ili mshahara wako usiingie ktk mfuko uliotoboka toboka. Japo shetani naye hajalala usingizi anasubiri mlangoni ili akuzuie usipate baraka kutoka kwa Mungu uzidi kumtumikia kwani ukianza kujiandaa tu kutoa zaka na yeye yuko anakupa mipango mingi ya matumizi ya kipato chako( anakupangia budget ya mwezi mzima pamoja na ile zaka uliyokuwa utoe hivyo unabaki mtupu) au kama ni vitu anakwambia kuwa hiki utakihitaji tena baadae au ni kizuri sana huwezi kukitoa hivyo unamtolea Bwana vile vilivyo dhoofu. Tunahitaji maombi ili kuweza kuvuka katika hili eneo hili  kwani limewakalia watu wengi na wengi wetu tupo kwenye vifungo katika hili swala. Bwana Mungu atuhurumie na atuwezeshe tuwe na moyo wa utoaji wa zaka na dhabihu kwa moyo mkunjufu.
MAOMBI YA KUMAANISHA NDIO YATAKAYOWEZA KUTUWEZESHA KULISHINDA HILI JARIBU.