Tuesday, November 16, 2010

MAOMBI YANGU KWAKO SIKU HII YA LEO

BABA KATIKA JINA LA YESU KRISTO NALITUKUZA JINA LAKO NA NINAKUSHUKURU KWA WEMA NA FADHILI ZAKO UNAZONITENDEA NDANI YA MAISHA YANGU SIKU HADI SIKU. ASANTE KWA UPENDO WAKO, ASANTE KWA REHEMA ZAKO, ASANTE KWA KUNIPA TUMAINI SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU, ASANTE KWA ULINZI WAKO NA BARAKA ZAKO UNAZONIPA SIKU HADI SIKU. LIHIMIDIWE JINA LAKO.

NAKUSHUKURU MUNGU WANGU KWA AJILI YA BABA HUYU, MAMA HUYU, KIJANA HUYU, BINTI HUYU NA WALE WOTE WATAKAOFUNGUA MAOMBI HAYA KWA MAANA MUNGU UMEZIDI KUWAPENDA KWA JINSI YA TOFAUTI. ENDELEA BWANA KUONYESHA UWEZA WAKO NA PENZI LAKO NDANI YA MAISHA YAO. WASAMEHE MAKOSA YAO BWANA NA UWAREHEMU NA KUWAHURUMIA, DAMU YA YESU KRISTO ULIYOMWAGIKA PALE MSALABANI KWA AJILI YA ONDOLEO LA DHAMBI IWATAKASE DHAMBI ZAO NA KUWASAFISHA NA KUWAWEKA HURU. USIWAACHE MFALME WANGU WA AMANI BALI WAZINGIRE KWA WIGO WAKO NA UTUKUFU WAKO UWAFUNIKE. ROHO MTAKATIFU  WAFUNIKE KWA WIGO WA MOTO WAKO UTAWALE NYUMBA ZAO, FAMILIA ZAO, WATOTO WAO, NDOA ZAO NA HATA KAZI ZA MIKONO YAO. USIWANYIME BARAKA ZAKO KILA IITWAPO LEO BWANA WANGU TEMBEA NAO KATIKA MAISHA YAO YA KILA SIKU KILA WAINGIAPO NA WATOKAPO WAKAPATE KIBALI MACHONI PAKO NA KWA WANADAMU PIA EE MWOKOZI WANGU. WAPE ILE HAJA YA MIOYO YAO BWANA KWANI WANAKUTUMAINIA WEWE TU KWA MAANA WEWE NDIWE NGAO YAO, NGOME YAO NA MSAADA KATIKA MAISHA YAO NA BILA WEWE BWANA HAWEZI KUFANYA JAMBO LOLOTE KWANI WEWE NDIO TEGEMEO LAO KUU.
WAKINGE NA KILA NGUVU ZA GIZA NA MAJARIBU YALETWAYO NA YULE MWOVU. WAOKOE KATIKA VISHAWISHI, KILA ROHO ZITAKAZOINUKA JUU YAO SIKU HII YA LEO NA ZISHINDWE KATIKA JINA LA YESU, NAKATAA ROHO YA HOFU NDANI YA MAISHA YAO KATIKA JINA LA YESU, NAKATAA MAGONJWA, NAKATAA ROHO YA UCHUNGU, HASIRA, CHUKI , KUKATA TAMAA KATIKA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARET ALIYE HAI. KIFUNGO KIWAYO CHOTE WALICHOFUNGWA NDANI YA MAISHA YAO NINAKIFUNGUA SASA KATIKA JINA LA YESU, NINAWAKOMBOA KATIKA ULIMWENGU WA KIROHO NA KUWARUDISHA POPOTE WALIPOFUNGWA KATIKA JINA LA YESU. SHETANI HANA MAMLAKA NAO, NGUVU ZA GIZA HAZINA MAMLAKA NAO, WACHAWI HAWANA MAMLAKA NAO, MAJINI HAYANA MAMLAKA NAO KUANZIA SASA, KUANZIA LEO KATIKA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI.
NAWAPA AMANI YA KRISTO, UPENDO, FURAHA, TUMAINI, AFYA NJEMA NA KILA HALI YA UWEZA WA MUNGU KATIKA MAISHA YAO YA KILA SIKU KUANZIA SASA. UWEPO WAKO BWANA USIWAPUNGUKIE BALI UZIDI KUWAFUNIKA NA KUWAONGOZA KILA WAKANYAGAPO WAPAMILIKI MUNGU WANGU. ROHO YA UNYENYEKEVU IUMBIKE NDANI YA MAISHA YAO, TUNDA LA ROHO MTAKATIFU LIUMBIKE NDANI YAO BWANA. ROHO MTAKATIFU TAWALA MAISHA YAO, ONEKANIKA BWANA NDANI YA MAISHA YAO. USIWAACHE JEHOVA BALI UZIDI KUWATUMIA KAMA CHOMBO CHAKO KITEULE. FANYA JAMBO JIPYA NDANI YA MAISHA YAO SASA BWANA, ANZA NAO KWA UPYA LEO TENA BWANA.
NAKUSHUKURU MUNGU WANGU, NASEMA ASANTE ROHO MTAKATIFU KWA MAANA MAOMBI HAYA YAMEKUBALIKA MBELE ZAKO NA YAMEKUWA MANUKATO KATIKA KITI CHAKO CHA ENZI EE MUNGU WANGU.
KATIKA JINA LA MWANAO MPENDWA YESU KRISTO NINAOMBA NA KUSHUKURU.

AMENI!  AMENI!  AMENI!

NENO LA UZIMA (KUBALI KUJARIBIWA)

Zekaria 13:9

Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha katika moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; WATALIITA JINA LANGU, NAMI NITAWASIKIA; mimi nitasema, WATU hawa ndio wangu; nao watasema BWANA NDIYE MUNGU WETU.

Haya si maneno yangu bali ni maneno ya Bwana Mungu akituambia sisi wana wake wa leo. Mpendwa kubali kupitishwa katika moto kwa maana lipo kusudi la Mungu kufanya hivyo. Ukiona vita vimekuwa vikali ndani ya maisha yako basi usimlau shetani wala usimnung'unikie Mungu kwa kudhania ya kuwa amekuacha ila ujue kuwa Mungu anakupitisha katika moto ili usafishwe kama fedha isafishwavyo utolewa kila aina ya uchafu, visiki hata vile vilivyoweka mizizi yake kwenda chini sana, (kwa maana ya udhaifu wako fulani ambao umekuwa ni vigumu kuuacha ambapo unakupelekea kutenda dhambi) hivi vyote anataka aving'oe ndani ya maisha yako, ili uwe safi. Kisha anakupitisha katika majaribu kwa maana ya kuwa anamwachia shetani akujaribu ili aone kweli umetakata unafaa kuwa chombo chake kiteule.
Majaribu ni mtaji mpendwa wa kukupeleka hatua nyingine katika ufalme wa kiroho, kusudi la Mungu kukupitisha katika moto na pia kuacha ujaribiwe ni kukusafisha na kukufanya uwe safi kama yeye alivyo kwani Mungu wetu hakai mahali palipo pachafu kwa sababu yeye ni Mtakatifu. Na ili wewe uwe Mtakatifu kama yeye alivyo ni kwa kusafishwa ndio maana anasema katika maandiko yake kuwa iweni watakatifu kama mimi nilivyo Mtakatifu. Sasa je wawezaje kuwa Mtakatifu kama bado unao uchafu ndani yako? Na hakuna awezaye kuuona uchafu uliokuwa nao isipokuwa yeye pekee ndiye aonaye hata ndani ya mioyo yetu na yeye ndiye anayeweza kukutoa yale ambayo kwa macho ya  nyama ya kibinadamu hatuwezi kuyaona ambayo yamekuwa changamoto kubwa katika maisha yako na kufanya usiweze kutumiwa na Bwana au yamekuwa kizuizi kikubwa cha wewe kufanikiwa. Kutokuwa msafi pia ndipo kunakopelekea hata maombi yako yanakuwa hayapokelewi kwa maana ukimwita Mungu anakuwa hakusikii maana anasema akishakusafisha na kukujaribu na kukuona safi ndipo utakapomwita jila lake naye atasikia.
Ukisoma katika 1Wakoritho 10:12 utaona ya kuwa Mungu ni mwaminifu hata akiaacha ujaribiwe anafanya pia na mlango wa kutokea katika hilo jaribu. Hivyo basi Mungu haruhusu majaribu yakupate kama hana kusudi jema nawe anachotaka ni wewe kumtumainia na kuamini kuwa anaweza kufanya yasiyowezekana yakawezekana cha msingi ni kuzidi kulitukuza jina lake, kumsifu na kushika maagizo yake na kutenda hasa hasa pale unapokuwa umepitishwa kwenye moto.
Faida ya kukubali kupitishwa kwenye moto na kujaribiwa ni kuwa utakapoita jina lakeanasikia tena kwa haraka sana anasema kuwa hakika utasema Bwana ndiye Mungu wako kwani atakutendea mpaka yale ambayo uliyokuwa hukuyaomba. Atafungua madirisha ya mbinguni na baraka zake zikushukie atakubariki uingiapo na utokapo, atabariki watoto wako, ndoa yako na hata familia yako kwa ujumla. Hata sahau kazi ya mikono yako kwani nayo pia itabarikiwa, atabariki mifugo yako na mazao yako shambani. Ukisoma katika Isaya 65:20-25 utaona ahadi nyingine za baraka kutoka kwa Mungu na ni jinsi gani utakavyoweza kufanikiwa katika maisha yako ukikubali kusafishwa.
Mungu wetu analokusudi jema nawe mpendwa kwani anakuwazia yaliyo mema siku zote. Hivyo basi kubali kupitishwa katika moto usafishwe uwe safi nawe uuone mkono wa Bwana ndani ya maisha yako.

NENO LA MUNGU LIGONGELEZEWE KATIKA VIBAO VYA MIOYO YETU.